Ni zamu ya YP na Y-Dash – TMK Wanaume
Baada ya TMK Wanaume kuwatoa wasanii Chege na Stiko sasa ni zamu ya YP na Y-Dash ambao hivi sasa wako kambini kukamilisha albam yao ambayo inatarajiwa italitetemesha jiji ile mbaya kwani vijana wako gado na hakuna asiyejua kuwa wana uwezo kisanii.
Baada ya TMK Wanaume kuwatoa wasanii Chege na Stiko sasa ni zamu ya YP na Y-Dash ambao hivi sasa wako kambini kukamilisha albam yao ambayo inatarajiwa italitetemesha jiji ile mbaya kwani vijana wako gado na hakuna asiyejua kuwa wana uwezo kisanii.
Akizungumza na Bongo5.com meneja wa kundi hilo Saidi Fellah alisema sasa hivi tunakuwa tunahitaji kujichimbia zaidi na kujipanga kwani muda wa kubahatisha umeshapitwa na wakati, hivyo vijana mpaka sasa wamesharekodi ngoma sita za ukweli nab ado wanarekodi taratibu na kwa uhakika zaidi
Wakati mabwana wadogo hao wanajipanga kambini humo mtu mzima Temba nae anavunja rekodi kwa kukamilisha albam yake yenye nyimbo 14, lakini anachokifanya ni kuwapa nafasi wasanii wenzake YP na Y-Dash, wakishatoka nae atatoka kwa kasi ya ajabu.
Bofya hapa kuangalia video ya “Pumzika” ya YP na Y-Dash.