Burudani
Nick wa 2 na Joh Makini waanzisha style mpya ‘Viburi Flow’
Huenda ukawa umejiuliza kidogo ile style waliyotumia ndugu kwenye hip hop Tanzania, Joh Makini na Nick wa 2 kwenye wimbo wao mpya ‘Bei ya Mkaa’.
Ile ni style mpya na wanaiita ‘Viburi Flow’.
“Viburi flow….ndio kitu Weusi tuna introduce 2013… ndio zilizo pigwa kwa Bei ya Mkaa,” ametweet Nick wa 2.
Naye Joh Makini alisisitiza kwa kuandika “Nikumbatie ‘am ready to fly’ bei ya mkaa’uumbaji wa michano mipya hata kama hamuongei mnasikia VIBURI FLOW.”