Nicki Minaj akasitisha show ya Uingereza kutokana na matatizo ya kiafya
First Lady wa Young Money Nicki Minaj amekuwa akifanya show non-stop katika miezi ya hivi karibuni lakini sasa inaonekana kama zimeanza kumwathiri.
Rapper huyo wa “Beez In The Trap” amelazimika kusitisha moja ya show zake za nchini Uingereza kutokana na sauti yake kuathirika.
Kwa mujibu wa mtandao wa Huffington Post, mwakilishi wake ametuma email inayosema kuwa Nicki atatakiwa kupumzika kuperform kwenye tamasha la siku mbili la V Festival kutokana na kile alichosema “strained vocal chords”.
Hivi karibuni Nicki alifanya show ya bure jijini New York iliyodumu muda wa saa mbili.