Burudani
Nicki Minaj atangaza tour yake ‘NICKIHNDRXX’, aungana na Future
Nicki Minaj ametangaza ujio wa ziara yake ya kimuziki NICKIHNDRXX Tour 2018/2019.
Msanii huyo wa kike ambaye anatajwa kuwa malkia wa muziki wa Hip Hop, ametaja ziara hiyo kuanza Septemba 21 mwaka huu ambapo itazunguka Marekani na Ulaya.
Ziara hiyo inatarajiwa kuanzia kwenye mji wa Baltimore na kufikia tamati Machi 28, 2019 mjini Geneva.
Kwenye ziara hiyo Nicki ametangaza kuungana na rapper Future. Wakati huo huo mashabiki wanasubiria kwa hamu kubwa albamu mpya ya mrembo huyo inayoitwa ‘Queen’ ambayo ametangaza kuiachia Oktoba 8, mwaka huu.