Habari
Nicolas Maduro ashinda uchaguzi kwa kishindo Venezuela
Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ameshinda tena kiti cha Urais kuiongoza nchi hiyo kwenye uchaguzi uliofanyika Jumapili hii.
Kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi huo yaliyotangazwa na rais wa tume ya uchaguzi wa nchi hiyo, Tibisay Lucena, Maduro amepata jumla ya kura milioni 5.8 wakati mpinzani wake Henri Falcon akipata kura milioni 1.8.
Jumla ya kura zote zilizopigwa zilikuwa ni milioni 8.6. Kwa mujibu wa matokeo hayo yanamfanya Maduro kuendelea kuingoza nchi ya Venezuela kwa kipindi cha miaka siata ijayo.
Maduro alianza kuiongoza nchi hiyo March 5, 2013 akichukuwa nafasi ya Hugo Chávez aliyefariki dunia.