Burudani
Niko sawa tu – asema Collo kwenye picha akiwa na noti za kutisha za dola mia mia!
Rapper wa Kenya, Collo anaweza kuwa amepotea kwa kiasi kwenye mawimbi ya redio na TV licha ya kuwa na ngoma mpya za hapa na pale, lakini haimaanishi kuwa amepigika.
Pengine anataka kudhihirisha hilo kwa mashabiki wake ndio maana ameamua kupost picha Instagram akiwa ameshika lundo la kutisha la noti za dola mia mia!
“Sina ubaya na mtu mimi. Niko sawa tu,” ameandika Collo kwenye picha hiyo.