Burudani

Nilitaka kumzuia asishiriki

Genevieve Mpangala Miss Tanzania 2010 na baba yake Emmanuel Mpangala

 

Baba mzazi wa Miss Tanzania 2010, Genevieve Mpangala, Emmanuel Mpangala ambaye ni Meneja wa timu ya Yanga amesema nusura amzuie mwanae kushiriki mashindano hayo kutokana na hofu kuwa ataharibikiwa.

Mpangala alimpongeza mwanae kwa ushindi huo “Nilikuwa sitaki lakini baadaye mimi na mama yake tuliamua kumruhusu na kumpa baraka zote”.

“Najua kwa sasa ameingia katika ulimwengu wa watu maarufu hivyo atakuwa anamulikwa na vyombo vya habari, naamini ataendelea kuwa mwema katika jamii. Nasi wazazi tutaendelea kumshauri juu ya maisha yake mapya” alisema Mpangala.

Mpangala ametangaza kumpa Genevieve zawadi ya nyumba anayomiliki iliyo katika kitongoji maarufu cha jiji la Dar es Salaam.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents