Michezo
Nimenusurika kifo kisa kuwapokea Plateau, kama mwizi – Shabiki asimulia mkasa mzima (+Video)
Baada ya video ya shabiki huyu wa #yangasc kusambaa kwenye mitandao ya kijamii ikionyesha kufanyiwa vurugu na wanaodaiwa kuwa ni mashabiki wa #simbasc Bongofive Tv imemtafuta @akilimalimakame21 na kuzungumza naye kwa kile kilichomfika siku ya Jumamosi Uwanja wa Mkapa baada ya kumalizika kwa mchezo wa Mnyama @simbasctanzania dhidi ya Plateau United
”Nimenusurika kifo, sauti zilikuwa zinasikika mkawasindikize mkawasindikize, nimeruka juu ya gari hata sijui nimewezaje. Mshabiki wa #simbasc ameniokoa ameniambia nipande juu ya gari la Tanesco.”- Akilimali Makame.