Habari
Nina huu ushauri kwa Rais Magufuli – Hamorapa
Harmorapa amefunguka na nia ya kutoa ushauri kwa Rais Magufuli juu ya mambo ambayo angependa kuona Rais anayafanyia kazi.
Harmorapa akiwa kwenye kipindi cha Kikaangoni kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV amemshauri Rais Magufuli kuboresha zaidi miundombinu.
“Rais Magufuli unajua yeye ndiye mwenye nchi sasa, hivyo mimi namuomba aboreshe zaidi suala la miundombinu natambua amefanya mambo mengi na makubwa kwenye sekta hiyo ila aboreshe zaidi, lakini pia namuomba Rais Magufuli aendelee kuwafinya wale wajanja wajanja kama ambavyo anafanya saizi na kingine atuangalie na sisi wasanii na kazi zetu” alisema Harmorapa
Na Emmy Mwaipopo