Burudani

Nipo katika wakati mgumu, naapa sihusiki na kusambaza video – Nandy

Baada ya hapo jana Nandy kuwaomba radhi mashabiki wake kutokana na kusambaa kwa video iliyomuonyesha akiwa faragha na aliyekuwa mpenzi wake. Leo, April 13, 2018, Nandy amesema hausiki na kusambaa kwa video hiyo.

Nandy amesema video imesambaa kutokana na kubadili simu mara kwa mara yeye pamoja na Bill Nass na ni kitu ambacho kinaweza kumkuta yeyote. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

Kiukweli niko katika wakati mgumu wa maisha yangu.. jana sikuwa sawa ila leo nimeweza hata shika simu yangu najuaa matusi yote na fedhea kutoka kwa mashabiki wangu ni sababu wanaamini hili ni kusudio letu au langu hii video iwe public naapa na naumia sana sana kwa hili lilitokea!!! sihusiki na kusambaza video wala siwezi ruhusu kitu kama hichi kitokee kwenye maisha yangu ya usanii hata ya kawaida!

Sitakiwi kujieleza sana ila naamini nikiandika hili nitakaa na amani kwa ambaye ataamuaa kuendelea kuni hukumu aendelee tu kunihukumu kwani kweli nimekosea ila ajiulize kama yeye hajawahi kukosea! Mambo yetu wote ya private yanatakiwa kubaki private, aliyeyatoa amefanikiwa kuleta hii taharuki, sintofahamu na maumivu makubwa ambayo sijawahi kupata maishani mwangu. ilaa Naamini sababu kuu ya hii video kuwa out ni mambo ya simu zetu ambayo inaweza kumtokea mtu yoyote!! nilibadili simu yangu mara 2 toka 2016 na bilnas aliibiiwa simu yake huko nyuma, kwa mujibu wake.

So hatujui mpaka sasa imetoka kwa simu ya nani? maswali ni mengi matusi ni mengi simu na sms ni nyingi mnoo… naumiaa naumiaa kupita kiasi. Kanisaa langu, wazazi wangu, ndugu zangu, marafiki zangu wa karibu wameliaa sana sanaa mnoo!!! sikatai nimerecord video na nilikuwa kwenye mahusiano na nilifanya kwa mapenz ila siwez weka public, Mungu anisamehe kwa niliyowakwaza. nimepoteza watu wa maana nahisi ku poteza vitu vingi ilaa nashukuru sana kwa watu wangu wa karibu waliolia na mimi mashabiki wanaoniamini Mimi na dhamira yangu ya kweli.

Marafiki walio liaa kwa ajili yangu nawashukuru sana mnoo yote naomba radhi sana sanakwa kilicho tokea haikuwa kusudio langu na naumiaa sana!!! asante sana basata kwa ushirikiano wenu kwakuwa na mm na kunipa moyo hii ni fundisho kwa wote nimejifunza kitu kikubwa sana!! mashabiki, kabisa langu, serikali yangu viongozi wenye imani na mimi, mashabiki zangu, ndugu jamaa na marafiki. naomba Nisameheni naamini na hili nalo litapita. Sitaongea tena kwenye vyombo vya habari kuhusu hili namwachia Mungu, pale roho yangu itakapopata wepesi tutaonana tena kwenye Sanaa. Naomba mniombee nipate wepesi wa kuvuka hili daraja.

Kwa upande wa Bill Nass hapo jana alieleza kilichotokea kwa upande wake kuhusiana na tukio hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram ila baada ya muda mfupi alifuta ujumbe huo ambao kwa asilimia kubwa ulitupa lawama kwa Nandy.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents