Burudani
Nisher asema umri unamfanya afikirie kuoa
Mtayarishaji wa video za muziki nchini, Nisher amesema anafikiria kuoa.
Nisher ambae yupo kwenye mapumziko katika kazi yake ya kutayarisha video, ameiambia Bongo5 kuwa wazazi wake wameanza kumuuliza kuhusu kuoa.
“Umri wangu unaenda,” amesema. “Natakiwa nianze kujiandaa kuoa, yaani nina mambo mengi. Familia yangu inaniangalia, wazee wangu wameenda umri umekuwa mkubwa, wanataka mjukuu, kwahiyo natakiwa nianze kujitenga,” amesisitiza.