Habari
Nisher kudirect video ya Press Play ya Dj Choka
Kama hujabahatika kusoma jarida la Mzuka la mwezi December mwaka jana ambalo lipo chini ya Bongo5 Media Group utakuwa unakosa mengi ya kumfahamu Nisher wa Arusha.
Ni kijana mwenye vipaji vingi na sasa umaarufu wake unazidi kuongezeka katika uongozaji wa video za muziki nchini.Tayari amechukuliwa kufanya video ya wimbo wa Dj Choka aliowashirikisha Gosby, Mabeste, M-Rap na Vanessa Mdee uitwao Press Play.
“Video ya PRESS PLAY Mungu akipenda inaweza kutoka tarehe hii 31.1.13 tuombe uzima tu. Dir by Nisher Bybee from Arusha #teamBhitz2013,” wameandika B’Hits.
Bila shaka huu ni mwaka wa Nisher kama tulivyotabiri kwa kusema ‘Nisher: The Next Big Thing’!!