Nitazidi kuwa juu!
Ray C ameibuka na kusema hata waje wasanii wangapi wa kike lakini anaamini hakuna kama yeye kamwe na hakuna atakayekuja kumfunika, alichonga hayo baada ya kudai siku za karibuni wameibuka wasanii wengi wa kike na kila mmoja kujitamba kwamba yeye ni zaidi ya wengine wote.
"Unajuwa watu wakikuona umekaa kimya wanadhani labda unawaogopa au vipi?, hawajui hata mtu kuwa unafanya nini, ni kweli kwa kipindi kirefu nilikuwa kimya lakini nilikuwa nafanya mambo yangu mengine nje ya nchi ambayo hayahusiani na muziki kabisa, basi wameibuka wengi na kashfa kibao, sasa nataka kuwaambia ya kuwa inatosha, na rasmi wajuwe kuwa mwaka 2010 nitakuwa kimuziki zaidi" alisema Ray C.