Noorah aingia mkataba na B-Hits
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Noorah a.k.a baba styles aliyepata kutamba na kibao chake cha ice creem ambacho ndicho kilichomtambulisha kwenye gem huku katika kibao hicho akiwa amemshirikisha Suma Lee kutoka kundi la park lane (kipindi kile)
Noora ambaye pia ni msomi wa mambo ya (IT) International Technology kutoka katika chuo kikuu cha IFM aliiambia bongo5
kuwa sasa hivi ameamua kurudi upya kwenye gemu kwa miguu yote miwili kwani ameshajipanga vya kutosha kabisa na ameshafanya ngoma kibao ambazo anatarajia kuziachia hivi akribuni huku akiwa amejikita katika katika studio za B Hits pande za namanga na projuza wa ngoma zake akiwa ni Pancho Latino.
“Nimejipanga vya kutosha kwani hapa nikisimama mimi mwnyewe, pale akisimama Pancho na kule akisimama mtumzima Hammy B naimani mambo yatakuwa yamesimama maana hii combination sio ya kitoto” alisema Noora.
Kwa upande mwingine Noorah ameweza kushirikiana vyema na mtu mzima Albart Mangwea katika ngoma ambayo ameiachia “katika hii project nimeweza kushirikiana vizuri na mwanangu Ngwea ambaye amefanya mambo kwenye hii ngoma”.
Kuhusu wasanii wangine Noorah alisema wala hawamtishi kitu chochote kwasababuya kile alichosaema kuwa yeye ndio baba stylehivyo anabadlika kutokana na wakati na mazingira. “mimi ujio wangu huu utakuwa utakuwa ni wa ukweli kutokana na nimebadilika kabisa na nimeenda na wakati uliopo japo huwa jamii hainelewi kwa haraka ila sasa hivi naamini nitaeleweka tu”.
Noorah kwa sasa amejikita katika na akiwa chini ya studio za B hits…