Msanii Noorah a.k.a The Baba’z kutoka kundi la Chamber Squad ameweka wazi kuwa alichokielezea ndani ya ngoma zai’ ni ukweli mtupu
Msanii Noorah a.k.a The Baba’z kutoka kundi la Chamber Squad ameweka wazi kuwa singo yake mpya inayokwenda kwa jina la zai’ kuwa alichokielezea ndani ya ngoma hiyo ni ukweli mtupu, kwani ni kweli alimzimia ile kinoma lakini huyo demu alikuja akamzingua.
Ni kweli nilimzimia sana huyo Zai na nilikuwa namfukuzia tangu tukiwa shule ya Sekondari Mazengo ambapo alinitangulia darasa moja, lakini pamoja na kumletea njaa zangu mtoto alimaliza shule na bado hakikueleweka kwani alitimua na kuniacha skuli, ndipo nikaamua kuandika ngoma hii ikiwa ni kama dedication kwake-Nooarah
Ilikuwa ni mwaka 2000 ambapo mtoto Zai alimaliza Shule na mpaka 2004 Noorah kilikuwa kinamsokonyoa akilini ndipo akaamua kuandika ngoma hiyo ambayo ameshirikiana na Mwanafalsafah, imerekodiwa ndani ya studio za Home Boy za nchini Kenya.
Source: Bongo5