Habari

Nukuu za Rais Magufuli akiwa ziarani Singida

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amezungumza mambo mbalimbali akiwa katika ziara mkoani Singida na leo amezindua barabara ya Manyoni – Itigi – Chaya yenye urefu wa KM 89.3.

Tazama nukuu zake hapa:

-Kabla sijaongea chochote naomba tuwaombee Mashujaa wetu walioitetea nchi yetu. Naomba tuiname tuwaombee.

-Watanzania naomba tuwe tunakumbuka mahali tulipo toka, mahali tulipo na mahali tunapoelekea.

-Tanzania ninayoipenda ni Tanzania yenye umoja, Tanzania yenye upendo, Tanzania inayomtanguliza mbele Mungu.

-Tunataka tuwe na umeme wa uhakika ili tuweza kuwa na Tanzania ya viwanda tunayoitaka.

-Wakati wa kukaa kwenye magenge na kushinda kwenye pool kukaa kupiga stori kwamba tutaletewa chakula cha bure, hakuna.

-Utajiri hautakuja kwa wavivu, lazima niwaeleze ukweli. Niwaombe wana Itigi wakati wa kukaa kwenye magenge umepita.

-Mimi ndiye Rais, hakuna anaejua siri za Serikali kama Rais. Leo mmepata Rais anaewaambia ukweli.

-Kosea hata kuoa, utatoa hata talaka ila usije ukakosea kuchagua.

-Ukiona mtu anapiga kelele wananchi wake waendelee kuwa masikini ujue amemeza kitu ndani.

-Kazi ya kutumbua ni ngumu unaweza ukajikata, unaweza ukarukiwa na usaa . Inadepend hilo jibu limekaa sehemu gani.

-Na leo watoto wote wanakalia madawati awe wa Chadema awe wa Tundu Lissu anakaa.

-Ni mataifa machache duniani yanayosomesha watu wake bure, hata Ulaya hawafanyi hivyo ndugu zangu.

-Ndege ya abiria 262 yenye uwezo wa kusafiri moja kwa moja kutoka Marekani inakuja mwakani.

-Waliojenga kwenye hifadhi ya reli waanze kujiandaa kisaikolojia, wanaweza kuanza kubomoa taratibu nyumba zao.

-Ma-DC na Ma-RC, sitoi chakula kama kwako kuna njaa, wilaya ikiwa na njaa wewe DC hufai kuwa DC, na wewe RC hufai.

-Nataka Tanzania iwe kama Ulaya. Tutafika tu lakini tutabanana.

– TanRoadS ni ya 3 kwa uchapaji kazi Afrika.

-Suala la ubinafsishaji mimi silipendi kabisa, siwezi nikawalaumu waliofanya hivyo, lakini kuacha kusema siwezi.

-Nikiondoka mimi hakuna atakayekuwa kama mimi, nasafisha njia ya Rais atakayekuja.

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents