Siasa

Nyalandu achukua fomu ya Urais: “Hatutawaweka watu kizuizini wawe CCM ama CHADEMA

Mtia nia Urais kupitia CHADEMA, @Lazaronyalandu akizungumza katika Makao makuu ya chama hicho Kinondoni, Jijini Dae es Salaam alipokwenda kuchukua fomu ya Urais.

“Kama nikipata nafasi ya kuteuliwa na chama changu natamani kuona umoja wa Kitaifa, naitamani Tanzania itaongozwa kwa katiba mpya, Katiba ambayo itadadafua mifumo iliyopita na kuifanya kuwa nchi yenye amani,umoja na mshikamano,

“Hatutawaweka watu kizuizini wawe wana ccm ama wanachadema wawe na madaraka ama hawana nyadhifa tunataka kuwa na haki pande zote ,naitamani Tanzania ambayo itakuwa nchi ya mfano wa mifumo imara ya utoaji haki thabiti ambao wakikatisha duniani popote wataonekana watu wa mfano”

“Ili tuiondoe ccm madarakani ni lazima umoja ndani ya chama chetu uwe imara,na muungano wa vyama vingine nao ukiwa imara,tutashinda si kwasababu tuna hasira ama tunataka kuwatoa ccm tunashinda kwakuwa tuna nia ya dhati ya kukomboa watanzania tunashinda kwakuwa tumedhamiria kuwahidumia watu”

https://www.instagram.com/p/CCYJkKQBWyY/

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents