Habari
Obama aacha sigara
Mke wa Rais wa Marekani, Michelle Obama amesema mume wake Barack ameacha uvutaji wa sigara.
Michelle akiongea na OK! Magazine ya nchini humo ameonyesha furaha kwa kitendo hicho cha mumewe kuonyesha mfano mzuri wa kuacha tabia hiyo ambayo ni hatari kwa afya yake. Michelle hakupenda kuongelea sana na kirefu na alimalizia kwa kusema, ‘mtu anapofanya jambo jema, basi inabidi umpe nafasi yake kuendelea kujitahidi,’
Rais Obama ambaye amewahi kusema kwamba hajawahi kuvuta sigara mbele ya wanao wala familia yake na ni kitu ambacho alikuwa akijitahidi sana kuacha katika siku za awali.