Burudani
Ochu aja Kuchakachua
Huyu ni msanii Ochu ambaye ameshatowa kazi zake mbili ya kwanza Dar es salaam na ya pili ambayo inafanya vizuri mpaka sasa ni Umechakachuwa.Kazihizo zote zimefanyika katika Studios za Seductive Records chini ya Producer Jilly ambaye kwa sasa yupo nchini kenya kikazi.
Nyimbo hizo zote zina Music Videos na zimetayarishwa na Director Solomon Lamba pale Emptysoulz Production, kwa sasa Ochu yupo mbioni katika kuandaa Music Video yake ya Tatu ambayo itakwenda kwa jina la Hofu ambayo anaamini itawashika zaidi na zaidi funs wake kwani kwa Tracks zake zilizopita watanzania wameonyesha kumpokea vya kutosha kiasi cha kuzipelekea Nyimbo na video zake kushika nafasi za juu east africa.