Burudani

Ofisi za THT zahamishwa Leaders Club Dar

Zikiwa zimepita wiki tatu toka aliyekuwa Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Vipindi Clouds, Ruge Mutahaba afariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu, Ijumaa hii Event ‘Coordinator’ wa Tanzania House Of Talent (THT) wamepanga kuhamisha ofisi ya THT ambayo ilikuwa Leaders Club Dar.

Ruge alikuwa anaitumia ofisi ya THT kama ofisi yake ya pili baada ya kufanya kazi kutwa nzima Clouds Media.

Rey ambaye ni Event ‘Coordinator’ wa Tanzania House Of Talent (THT) hajaeleza sababu ya kuihamisha ofisi hiyo.

Rey akiwa na Amini

“Tanzania House Of Talent (THT) itaendelea kuwepo, changamoto hazikosekani, tofauti na yeye alivyokuwepo, kwa sasa tumehama pale tulipokuwepo mwanzoni Leaders Club, tumehamia Mikocheni location tutaitaja baadae, lakini tunaendelea vizuri” Rey

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents