Michezo

Ole Gunnar Solskjaer amwagia sifa Paul Pogba ‘Huyu ndiye Paul ninayemfahamu mimi’

Kocha wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer amesema kuwa kiungo wake, Paul Pogba ameanza kurejewa na furaha huku akiamini kuwa kiwango alichokionyesha kwenye michezo yake ya hivi karibuni ndicho alichokuwa anakifahamu.

Paul Pogba took his shirt off and celebrated in front of the cameras after the victory

Pogba alikuwa moja ya zana muhimu kwenye ushindi wa hapo jana siku ya Jumatano huku akifanikiwa kutupia mabao mawili dhidi ya Huddersfield.

The Frenchman is happy again and can revive his Manchester United career, says his manager

‘ ‘Huyu ndiye Paul ninayemfahamu mimi, mtu ambaye namfahamu tangu tulivyo kuwa naye kipindi hicho,’’ Solskjaer ameongeza kuwa kwa sasa kijana huyo amekuwa mwenye furaha muda wote na tabasamu usoni.

The Manchester United midfielder has looked in superb form under Ole Gunnar Solskjaer

‘’Unapoichezea United unapaswa kuwa nafuraha, licha ya kuwa na majukumu lakini pia ni heshima kubwa.’’

‘’Paul anafahamu nini maana ya kuichezea Man United. Ametengeneza nafasi mbili hadi tatu na safari hii amefunga magoli mawili, nina hakika atafurahia,’’

‘’Tulipofunga bao la pili, uliona namna kujiamini kulivyoongezeka kwa wachezaji, huku nidhamu ikizidi kukua.’’

‘’Hatukufanya vyakutosha, ila wala huitaji kubadilikitu zaidi ya mitazamo ya wachezaji, nahitaji timu ipate matokeo.’’

Solskjaer thinks Pogba understands the privilege and responsibility of playing for the club

Solskjaer na kiungo huyo wa kati wanaonekana kuwa wenye maelewano huku meneja huyo anaamini Pogba mwenye umri wa miaka 25 ameanza na mwanzo mzuri Old Trafford.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents