Ole Gunnar Solskjaer amwagia sifa Paul Pogba ‘Huyu ndiye Paul ninayemfahamu mimi’
Kocha wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer amesema kuwa kiungo wake, Paul Pogba ameanza kurejewa na furaha huku akiamini kuwa kiwango alichokionyesha kwenye michezo yake ya hivi karibuni ndicho alichokuwa anakifahamu.
Pogba alikuwa moja ya zana muhimu kwenye ushindi wa hapo jana siku ya Jumatano huku akifanikiwa kutupia mabao mawili dhidi ya Huddersfield.
‘ ‘Huyu ndiye Paul ninayemfahamu mimi, mtu ambaye namfahamu tangu tulivyo kuwa naye kipindi hicho,’’ Solskjaer ameongeza kuwa kwa sasa kijana huyo amekuwa mwenye furaha muda wote na tabasamu usoni.
‘’Unapoichezea United unapaswa kuwa nafuraha, licha ya kuwa na majukumu lakini pia ni heshima kubwa.’’
‘’Paul anafahamu nini maana ya kuichezea Man United. Ametengeneza nafasi mbili hadi tatu na safari hii amefunga magoli mawili, nina hakika atafurahia,’’
‘’Tulipofunga bao la pili, uliona namna kujiamini kulivyoongezeka kwa wachezaji, huku nidhamu ikizidi kukua.’’
‘’Hatukufanya vyakutosha, ila wala huitaji kubadilikitu zaidi ya mitazamo ya wachezaji, nahitaji timu ipate matokeo.’’
Solskjaer na kiungo huyo wa kati wanaonekana kuwa wenye maelewano huku meneja huyo anaamini Pogba mwenye umri wa miaka 25 ameanza na mwanzo mzuri Old Trafford.