Michezo
Olivier Giroud aingia kwenye vitabu vya rekodi za Arsenal
Mshambuliaji wa klabu ya Arsenal na timu ya tafifa ya Ufaransa Olivier Giroud baada ya kufunga wikiend hii amefikisha idadi ya magoli 50 katika ligi ya EPL goli hilo la mkwaju wa penati katika mchezo dhidi ya Aston Villa baada ya Alan Hutton kumvuta Theo Walcott kwenye eneo la box.
Giroud alifunga mkwaju huo wa penati na kufikisha magoli 14 msimu huu na kuwa mchezaji wa saba wa Arsenal kufunga magoli 50 kwenye ligi ya EPL wakati yeye ikimchukua michezo 113 kufikia rekodi hiyo.
Wachezaji wengine ambao wamewahi kufikisha magoli 50 kwenye mechi za ligi ya EPL wakiwa wanaitumikia Arsenal ni pamoja na Thiery Henry, Ian Wright, Robin van Persie, Dennis Bergkamp, Robert Pires, Theo Walcott na mwenyewe Olivier Giroud.