Habari
Orodha ya wasanii watakaotumbuiza kwenye uzinduzi wa kombe la mataifa ya Africa – 2013
Wasanii 9 wamepewa shavu la kutumbuiza kwenye sherehe za uzinduzi wa kombe la mataifa 2013 nchini Afrika Kusini.
Wasanii hao ni pamoja na Oumou Sangare wa Mali , Eric Wainana wa Kenya, Judith Sephuma, Lira, Siphokazi, Ayanda Nhlangothi Afurukan, Sipho ‘Hotstix’ Mabuse na Ringo Madlingozi wa Afrika Kusini.
Ufunguzi huo wa The Orange Africa Cup of Nations SOUTH AFRICA 2013 utafanyika Jumamosi hii, 19 January kuanzia saa kumi jioni kwa saa za Afrika Kusini. Utafuatiwa na mechi ya Bafana Bafana na Cape Verde.