Burudani

P-Funk amtabiria makubwa Harmorapa

Mtayarishaji mkongwe wa muziki nchini P-Funk Majani amemtabiria makubwa makubwa Harmorapa.

Kutoka Kushoto: Harmorapa, Chin Bees na P-Funk Majani

Akiongea kwenye kipindi cha FNL cha EATV wakati wa kutambulisha video mpya ya rapper huyo chipukizi, Majani amesema, “Mtu mwenye busara kama huyu kijana lazima umbless, is a special kid.”

“The way he listen and the way he speaks the people ana heshima kubwa mno ambayo mimi sijawahi kupata kwa wasanii wengine. Anataka kujifunza, anataka kujua zaidi habahatishi na hafanyi muziki kwa sababu ya kutafuta kiki no he is gonna be big, trust me. Kila mtu anaanza anatambaa baadaye unaanza kushika kochi lile kidogo unadondoka unainuka, unainuka then unaanza kidogo kukimbia na unatembea kidogo halafu unaanza kukimbia kabisa unakuwa mwanariadha.,” ameongeza.

“Maisha ndiyo hivyo, kumbuka Sam mimi hawa watoto wote ambao wana majina makubwa wameanza wapi? Nimewaona wakikua exactly, so mimi najua vipaji,” amesisitiza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents