Burudani

“Pambano la Floyd Mayweather na kickboxer mwenye umri wa miaka 20 bado lipo” – Nobuyuki Sakakibara

Pambano la Bondia wa Marekani Floyd Mayweather na ‘kickboxer’ mwenye umri wa miaka 20 Tenshin Nasukawa bado litafanyika usiku wa Mwaka Mpya kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya uendelezaji wa kuandaa matukio ya martial arts.

Kumbuka kuwa mwanzoni mwa mwezi huu, Mayweather mwenye umri wa miaka 41 alitangaza kupambana na kickboxer huyo katika mkutano alioufanya na waandishi wa habari huko Tokyo, lakini baada ya kushambuliwa kwa maneno na watu wengi, Mayweather alikanusha uwepo wa pambano hilo akisisitiza kwamba yeye alikubali tu pambano hilo liwe na raundi tatu mbele ya kundi dogo la matajiri (watazamaji) kwa dau kubwa sana.

Sasa kutokana na taarifa kutoka kwa mkurugenzi wa Rizin Fighting Federation Nobuyuki Sakakibara kupitia mtandao wa Twitter, Sakakibara ametuhakikishia kwamba pambano hilo lipo na litafanyika tarehe 31 Disemba mwaka huu baada ya kutatua migogoro yao na Floyd Mayweather

“Migogoro na Floyd Mayweather imetatuliwa” Sakakibara aliandika hivyo katika tweet aliyoituma leo Ijumaa ikiambatana na picha ikimuonesha yeye na Mayweather.

‘Atapigana na Tenshin Nasukawa siku ya mkesha wa mwaka mpya kwa RIZIN 14. Nitaelezea maelezo zaidi mara tu! nitakaporudi Japan.’

Sakakibara anatarajiwa kuongea na waandishi wa habari siku ya jumamosi ya tarehe 16|11 mwaka huu .

Na Raheem Rajuu

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents