Michezo

Panucci apatakibarua cha kuinoa Albania

Beki wa zamani wa timu ya taifa ya Italia, Christian Panucci ameteuliwa na Chama cha soka cha nchini Albania (AfA) kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya nchi hiyo.

Panucci anachukua mikoba ya kocha wa zamani wa taifa hilo Gianni De Biasi, ambae alijiuzulu mwezi uliopita.

Raisi wa chama hicho cha soka Armand Duka amesema kazi ya kwanza ya kocha huyo mpya ni kufuzu kwa fainali za michuano ya Ulaya ya 2020.

Panucci aliwahi kuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Urusi chini ya Fabio Capell, pia amewahi kuvifundisha vilabu vya Livorno na Ternana vya Seria B na amewahi kuvichezea vilabu vya Real Madrid na As Roma.

By Hamza fumo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents