Burudani
Papa Dennis wa Kenya amvuta Ray C kwenye ‘Tordado’ (Video)
Mwanamuziki kutoka nchini, Kenya Dennis Mwangi aka Papa Dennis ambaye anafanya kazi chini ya record label ya Maliza Umasikini kaachiwa wimbo wake mpya Tordado akiwa amemshirikisha mwanadada Mtanzania Rehema Chalamila.
Wimbo huo unazungumzia mapenzi ambapo anaependwa kazidiwa na mahaba hadi anahisi
mapenzi yake ya nguvu kama kimbunga.
Video ya wimbo huu imetengenezwa nchini Afrika ya Kusini na muongazji wa video maarufu
sana God Father.
Mbali wimbo huo Papa Dennis ameshafanya nyimbo na vinara wengi wa muziki wa Africa
akiwemo Mr Flavour (Nigeria) ,Chiddimna (Nigeria) ,Korode bello (Nigeria) na sasa RAY – C.