Michezo
Papa Massata akamatwa kujihusisha na vitendo vya rushwa
Aliyekuwa rais wa shirikisho la riadha ulimwenguni, Lamine Diack amekamatwa na mwanae, Papa Massata Diack nchini Brazil kwa tuhuma za rushwa.
Aliyekuwa rais wa shirikisho la riadha ulimwenguni, Lamine Diack
Diack na mtoto wake wa kiume Massata Diack wanashutumiwa kwa tuhuma hizo nchini Ufaransa kwa kupokea dola milioni 2 kwa ajili ya kuufanya mji wa Rio kuwa muandaaji wa michuano ya Olimpiki mwaka 2016.
Papa Massata Diack
Awali wawili hao walikana mashitaka ya kuhusika katika vitendo vya rushwa, Lamin kwa sasa anashikiliwa nchini Ufaransa na tayari amenyanganywa hati yake ya kusafiria huku mtoto wake Papa Massata akiwa amejificha nchini kwao Senegal.