Michezo
Pato sambamba na Barca
Mshambuliaji wa Ac Millan anayetokea Brazil Alexandre Pato amesema licha ya kuhusishwa na kujiunga na klabu za England hususan Man City kama akiondoka alipo sasa, yeye atatua katika klabu ya Barcelona.
Pato aliyosajiliwa katika klabu hiyo inayotumia uwanja wa San Siro kwa dau la euro milioni 22 mwaka 2007, amekuwa akiwaniwa na klabu za Man City na Chelsea. Kuna uwezekano akaihama klabu yake Januari mwakani.
‘Nimekuwa nikiwaniwa na City lakini bado ni mchezaji wa Milan nafurahia kuwa hapa,kama siku nikiondoka nitalazimika kuivaa jezi ya Barcelona, hilo ndilo ninalolitegemea,’ alisema Pato.