Michezo
Patrice Evra ajiunga rasmi Juventus
Beki wa timu ya taifa ya Mfaransa Patrice Evra amekamilisha uhamisho wake kutoka Manchester United kuelekea Juventus kwa ada ya paundi milioni 1.2.
Evra mwenye miaka 33 amesaini mkataba wa miaka miwili na klabu ya Juventus ya Italia. “Kuichezea Man United ilikuwa nafasi ya kipeke, ndoto iliyokuwa kweli na nimetengeneza kumbukumbu nzuri,” alisema Evra.
Pia amemshukuru Sir Alex Ferguson kwa kumpa nafasi kuwa nahodha wa Manchester United na kuelewa kuwa hakuna kubwa kuliko klabu.