Michezo
Paul Pogba anamuhitaji Mourinho ilikurudi katika kiwango chake
Paul Pogba anahitaji msaada wa meneja wa Manchester United, Jose Mourinho ili kuondokana na kipindi hiki kigumu ndani ya Old Trafford.
Pogba ambaye ameweka rekodi ya usajili ndani ya United wa pauni milioni 89 amekuwa akisugua benchi huku Mourinho akimchagua Scott McTominay raia wa Uingereza kucheza na fasi ya kiuongo ambayo huchezwa na Mfaransa huyo katika mchzo dhidi ya .
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 nahitaji kupewa nafasi na Mourinho ilikuweza kuirudisha thamani yake tena.
Wakala wa mchezaji huyo, Mino Raiola ameanza kuchukua hatua za kutafuta klabu ya kwenda staa huyo wa United ambayo itakuwa tayari kutoa dau nono la usajili pamoja na kumlipa mshahara wa pauni 200,000 kwa wiki huku Real Madrid inahusishwa na kumsajili Pogba.