Paul Pogba awaambia watu wake wa karibu kwamba anataka kujiunga na Barcelona
Paul Pogba awaambia watu wake wa karibu kwamba anataka kujiunga na Barcelona
Kiungo wa kati wa klabu ya Machester United na raia wa Ufaransa Paul Pogba amewaaambia watu wake wa karibu pamoja na wachezaji wenzake kuwa anataka kuondoka Old Trafford na kujiunga na wababe wa Katalunya FC Barcelona.
Mfaransa huyo amekuwa na wakati mgumu katika klabu hiyo kwani msimu uliopita ilisemekana hawana uelewano mzuri na kocha wake Jose Mourinho,huenda ndo ikawa sababu ya kiungo huyo kutaka kuachana na Mourinho.
Lakini pia Pogba amekuwa na ukaribu na beki wa kati wa timu ya taifa ya Ufaransa na klabu ya Barcelona Umtiti kwani baada ya michuano ya kombe la Dunia kumalizika walionekana wakiwa wote nchini Marekana wakiwa mapumzikoni.
Licha ya kiungo huyo kutaka kuondoka Old Trafford,Manchester United walihusishwa katika usajili wa wachezaji kadhaa wakiwemo mabeki wa kati wa klabu za Leicester ambaye ni Henry Maguire,beki wa klabu ya Tottenham Toby Alderweireld pamoja na beki wa Bayern Munich Jerome Boateng,kwa taarifa za sasa hivi asubuhi beki huyo tayari amemjibu Mourinho kuwa hayuko tayari kuhama Bayern na kujiunga na Manchester.
Pogba alisajili na Manchester United kutoka Juventus kwa ada ya uhamisho wa Euro Mil 89,ikiwa ndio rekodi ya timu kununua mchezaji kwa gharama kubwa.
By Ally Juma
Tunamukalibicha mu team kubwa
Aje tuuuuuu
LA liga kweny sio ligi ya ushindani pale ni REAL , BARCA , ALTETICO bas ndo timu ambazo kila xku zinafika final kwaiyo akuna ushindani ukizingatia pale EPL kwaiy akaze tu na akitak kuam ni bora awe pale pal uingereza
Hatak ushindan huyu mwenzio bahs anahtaj mataj makubwa makubwa so anajua akiwa barca ndan ya misim 3 hakos kubeba uefa
Barca xjui kwaiy misimu mitatu kam watachukua ilo UEFA timu sasa ivi zinakaza kinoma
Ngoja tutaona
DILI LIMESHAKUFA POGBA HAUZWI TENA
Nenda kapoteee huko
Katka hawo watu wake wa karibu nitajie mmoja ambae amekwambia hii habari