Michezo
Paulo Dybala asaini mkataba mpya Juventus
Mchezaji wa klabu ya Juventus, Paulo Dybala amesaini mkataba mpya wa miaka mitano utakaomuweka Torino hadi mwaka 2022 atakuwa akilipwa Paundi 110,000 kwa wiki.
Paulo Dybala (kulia) akipeana mkono na Mwenyekiti wa Juventus, Andrea Agnelli (kushoto) baada ya kusaini mkataba mpya.
Amesaini mkataba mpya siku mbili baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 kufunga mabao mawili katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Barcelona kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya