Pedro Rodriguez atua rasmi Chelsea
Klabu ya Chelsea imeipiku Manchester United katika mbio za kumsajili Pedro Rodriguez, 28, aliyekamilisha uhamisho wake kutoka Barcelona kwa ada ya ya pauni mil 21.1 na mkataba wa miaka minne ndani ya Chelsea.
Pedro akiwa na mchezaji mwenzake wa zamani wa Barcelona Cesc Fabregas
Baada ya uhamisho huo kukamilika Pedro aliwajulisha mashabiki kwa tweet ya kuishukuru klabu ya Barcelona na pia akielezea furaha yake ya kujiunga na mabingwa hao watetezi wa ligi kuu nchini Uingereza.
“Naishukuru klabu ya Barcelona pamoja na Chelsea kwa kufanikisha uhamisho huu, ninatazamia kuendelea kushinda vikombe na klabu Chelsea,” alisema Pedro.
Vikombe ambavyo Pedro amewahi kushinda akiwa na klabu ya Barcelona
Pedro akifanya mazoezi na mlinzi wa Chelsea Cesar Azpilicueta kwenye uwanja wa Cobham