Michezo
Pellegrini na Andre Ayew watwaa tuzo ya mwezi ligi kuu ya Uingereza
Ligi Kuu ya Uingereza imemtangaza kocha wa Manchester City, Manuel Pellegrini kocha bora wa mwezi Ligi Kuu baada ya timu yake Manchester City kuanza vizuri msimu mwezi Agosti ambapo wameshinda mechi zote nne mfululizo.
Kocha wa Man City Manuel Pellegrini
Tuzo hiyo hutolewa pia kwa mchezaji bora wa mwezi na imeenda kwa Mghana Andre Ayew, 25 ambaye amekuwa na mwanzo mzuri Uingereza.
Andre Ayew akiwa na tuzo yake
Mchezaji huyo ameifungia Swansea magoli matatu tangu msimu uanze ligi Kuu.
.