Habari

Penzi linapobadilika na kuwa Heshima

Hili swala la penzi kwisha mimi huwa nalisikia tu kutoka kwa watu tofauti kuwa kuna wakati mtu unajikuta humpeni tena mpenzi wako na unatafuta namna ya kujitoa kwenye uhusiano wenu wa kimapenzi.

Hili swala la penzi kwisha mimi huwa nalisikia tu kutoka kwa watu tofauti kuwa kuna wakati mtu unajikuta humpeni tena mpenzi wako na unatafuta namna ya kujitoa kwenye uhusiano wenu wa kimapenzi.

 

Kwa wale waliko kwenye ndoa huwa ni ngumu kidogo kutokana na “dini” kuwabana au anabaki ndani ya ndoa uhusiano kwa vile anakuheshimu kwa kuwa ni mama wa watoto wenu hasa kama umemzalia watoto 2-3 hivi lakini ktk hali halisi anakuwa na mtu mwingine ampendae nje ya ndoa (part time lover a.k.a Kimada a.k.a nyumba ndogo).

 

Mwanamke unatakiwa kuwa makini na mjanja kutambua mabadiliko hayo(penzi au heshima), kwani mtu anapokuheshimu na kukuthamini kwa vile umemfanyia jambo fulani kubwa hakuna tofauti kubwa sana na kupendwa.

 

Hivyo ikiwa kila usiku analala kitanda kimoja na wewe nakukamilisha mambo mengine ya kifamilia na kuambiwa “nakupenda mama nanihii” haina maana kweli anakupenda bali anakuheshimu na vilevile anajaribu kuepuka malalamiko au maswali.

 

Mimi binafsi naamini kuwa unapompenda mtu kwa maana halisi ya mapenzi huwezi kuchoshwa au penzi lako kwake kupungua kama sio kwisha kabisa.
Pamoja na mambo mengine kuna sababu zinazochangia mabadiliko hayo ambayo ni kujisahau kwako mwanamke, kuwa na tabia ya “ndio bwana”, kukubali usemi kuwa “mumeo akiwa ndani akiwa nje si wako bali wa wote”, kukimbilia kuzaa siku chache baada ya kuwa ndani ya uhusiano au ndoa kwa vile unahofia usipompa mtoto basi ataenda kuzaa nje n.k.

 

Nakaribisha nyongeza kuhusu hili, maswali, maoni na ushauri…

 

Source: Dinahicious

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents