Michezo
Pep Guardiola Ataka Manchester City kuwasajili Paulg Pogba na John Stones
Kocha Pep Guardiola baada ya kutangazwa kuanza kazi mapemaa ndani ya kikosi cha Manchester City mwishoni mwamsimu huu katika majira ya Joto amewataka City ianze “kuvunja benki” mapema.
Guardiola ametaka City ifanye inavyoweza kumnasa kiungo Paulg Pogba wa Juventus.
Pogba anapatikana kwa kitita cha pauni milioni 80 na anawaniwa na timu vigogo kama Real Madrid, Chelsea na Barcelona.
Pamoja na Pogba pia Guardiola ameitaka City kuhakikisha inampata beki wa Everton, John Stones hata kwa kutoa pauni milioni 50 kumnasa.