Picha
Thamani ya nyumba mpya ya Peter wa P-Square iliyopo Marekani ni zaidi ya tsh bilioni 4!!
Pamoja kundi la P-Square kumiliki kwa pamoja nyumba ya kifahari nchini Nigeria iitwayo Squareville ambayo imejengwa kwa mabilioni ya shilingi, Peter Okoye ambaye ni mmoja wa mapacha hao ameonesha nyumba yake anayomiliki huko San Fransisco, Marekani.
Kwa mujibu wa vyanzo, thamani ya nyumba hiyo ni $2,750,000 ambazo ni zaidi ya shilingi bilioni 4 za Tanzania.
Katika picha inayoionesha nyumba hiyo aliyoiweka kwenye mtandao wa Instagram Peter ameandika “My little Squareville in San Fransisco ….. Thank u Lord.”
Tazama picha za ndani ya nyumba hiyo na uone jinsi hawa jamaa walivyo na utajiri.