Burudani
Picha: Abeneko apagawaisha tamasha la Barazani
Msanii wa muziki wa Asili Isack Abeneko maarufu kama Abeneko usiku wa jana ameweza kukonga mioyo ya wapenzi wa burudani kwa kutoa show kali katika tamasha la Barazani lililofanyika Alliance Fracaise.
Abeneko ambaye anafanya vizuri sokoni na albamu yake ya ‘Wakati’, alitoa show hiyo akiwa ameambatana na Bendi yake.
Pia msanii huyo amechaguliwa kwenda kuwakilisha Tanzania nchini Uganda kwenye tamasha kubwa la kimataifa la Bayimba Art Festival mwezi wa nane mwaka huu.