Picha: Arsene Wenger na Jose Mourinho walivyotaka kuzichapa uwanjani
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger na mwenzake wa Chelsea, Jose Mourinho almanusra wageuke Mayweather na Maidana kwenye mechi kali iliyofanyika Stamford Bridge kati ya timu hizo.
Kocha wa Arsenal, Wenger kushoto akisukumana na mpinzani wake Mourinho wa Chelsea
Wakati mechi ikiendelea ikiendela palitokea kutokuelewana baina ya makocha hao wawili baada ya Wenger kumfuata Mourinho na kuanza kusukumana baada ya beki wa Chelsea, Cahil kumchezea rafu Sanchez.
Mwamuzi akijaribu kuwaamua
Makocha hao walijikuta wakianza kusukumana na nakutokea mzozo hadi mwamuzi alipowafuata na kuwapa onyo kuwa wakiendelea atawatoa wote nje ndipo walipotulia. Mchezo uliisha kwa Chelsea kushinda 2-0.
Akiongea na waandishi wa habari, Wenger alisema hajutii kitendo hicho.
Mzozo huo uliteka hisia za watu wengi
Ubabe ubabe tu