Picha: Barack Obama ashuhudia mchezo kati ya Chicago Bulls na Cleveland Cavaliers
Rais wa Marekani Barack Obama alikuwa mmoja kati ya watu waliohudhuria mchezo kati ya Chicago Bulls dhidi ya Cleveland Cavaliers, alfajiri ya Jumatano hii kwa saa za Afrika Mashariki.
Huo ulikuwa sehemu ya mechi za ufunguzi wa ligi ya kikapu ya Marekani, NBA.
Obama ambaye ni shabiki mkubwa wa Chicago Bulls, alipata nafasi ya kushuhudia timu hiyo ikipata ushindi wa pointi 97-95 dhidi ya Cavaliers katika dimba la United Centre.
Wachezaji wengi akiwemo LeBron James na Derrick Rose walidai kuwa ni heshima kubwa kucheza mechi mbele ya Rais Obama.
Baada ya kushuhudia mechi hiyo, Obama aliandika kwenye Twitter:
Good to be home for a night. Even better to see the @chicagobulls start the season off right! #SeeRed
— President Obama (@POTUS) October 28, 2015