Burudani
Picha: Big Sean afunga mwaka kwa kununua jumba la kifahari
Rapper Big Sean anakaribia kuufunga mwaka 2017 kwa kuonesha jeuri ya fedha. Amenunua jumba la kifahari lenye thamani ya dola milioni 8.7 ambapo kwa fedha za kitanzania ni zaidi ya shilingi bilioni 19.5.
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, umedai mjengo huo ambao upo katika eneo la Beverly Hills, California unaukubwa wa eneo la mraba 11,000 sq, vyumba saba vya kulala, na mabafu 8.
Hizi ni baadhi ya picha za jumba hilo.