Bondia Manny Pacquiao aliweka gloves pembeni na kuonesha kipaji chake kingine na kuishangaza dunia kwa kucheza mpira wa kikapu Jumapili iliyopita ikiwa imebaki kama mwezi mmoja kabla hajapanda ulingoni kutetea mkanda wa WBO.
Pacquiao aliichezea KIA Sorento inayoshiriki ligi ya kikapu nchini Ufilipo.
Pacquiao mwenye umri wa miaka 35 alicheza kwa dakika saba, na kuisaidia timu yake kushinda kwa point 80 dhidi ya 66 dhidi ya Blackwater Elite kwenye cot ya Philippine Arena.
Pacquiao, amejiunga kwenye timu hiyo kama kocha mchezaji, lakini alicheza michezo ya kujiandaa na msimu mapema mwezi huu na kufanikiwa kufunga point moja. Pacquiao ana urefu wa futi 5 point 6, urefu ambao katika mchezo wa kikapu hauruhusu.