Bongo Movie
Picha: Bongo Movie Unity wazindua kilimo kwanza Kondoa, Dodoma
Katika kujiweka karibu na wananchi hivi karibuni wasanii wa Bongo Movie Unity waliitembelea wilaya ya Kondoa, Dodoma katika uzinduzi wa kilimo kwanza.
“Ni jadi yetu ya kufanya kazi za jamii juzi tulikwenda Kondoa kwa ajili kufanya uzinduzi wa Kilimo kwanza uliofanyika Kijijini Kwadelo lengo na dhumuni lilikuwa kwenda kuhamasisha mpango mzima wa vijana kuacha kuja mijini na kuwekeza kwenye kilimo,” aliandika Ray kwenye blog yake.
“Na kuanzia tu Serikali ilitoa Matrekta sitini na nne kama kianzio cha mradi huo.” Hizi ni baadhi ya picha za uzinduzi huo.