Picha: Cheki T-Africa walivyochukua ubingwa wa Dance 100% 2012
Washindi hao wa shindano hilo lililoandaliwa na kituo cha televisheni cha East Africa Television, wamejinyakulia zawadi ya fedha taslimu shilingi milioni 5.
Shindano hilo lilishirikisha makundi bora kutoka wilaya za Temeke, Ilala na Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Makundi yaliyoingia fainali ni pamoja na FBI, Best Friends, TZ Queens, The Chocolate na T-Africa