Picha: Cheki T-Africa walivyochukua ubingwa wa Dance 100% 2012

Kundi la T-Africa limeibuka na ushindi wa shindano la kucheza muziki la Dance 100% 2012 katika fainali iliyofanyika kwenye viwanja vya Leaders Club Kinondoni siku ya Jumamosi, August 11.
Washindi hao wa shindano hilo lililoandaliwa na kituo cha televisheni cha East Africa Television, wamejinyakulia zawadi ya fedha taslimu shilingi milioni 5.

Shindano hilo lilishirikisha makundi bora kutoka wilaya za Temeke, Ilala na Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Makundi yaliyoingia fainali ni pamoja na FBI, Best Friends, TZ Queens, The Chocolate na T-Africa

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents