Picha
Picha: Chismo aliyedai kuibiwa wimbo na Richie Mavoko ‘Follow Me’ aula
Msanii Chipukizi aliyewahi kuingia kwenye mgogoro mkubwa na Richie Mavoko kuhusu wimbo ‘Follow Me’ akidai kuwa ulikuwa wake, amepata shavu la kupewa mkataba wa usimamizi.
Chismo na Meneja wake Duwe Santana wakisaini mkataba
Chismo ambaye jina lake halisi ni Adam Mustafa ameingia mkataba na kampuni Machapta Inc itakayomsimamia kwa kipindi cha mitatu. Msanii huyo alianza muziki kama dansa na alishafanya kazi na wasanii kibao wakiwemo Bob Junior, Dully Sykes, Baby J, Tunda Man na Richie Mavoko.
Akiwa kwa Richie, anasema ndiko wimbo wake Follow Me ulioibiwa kwakuwa alikuwa akiuimba mbele yake.
Chismo ashikana mkono na Mkurugenzi wake Mwinyi Machapta