Picha: Clouds watangaza ujio mpya wa Tamasha la Tigo Fiesta 2019
Lile Tamasha kubwa la muziki nchini Tanzania Tigo Fiesta linatarajia kuanza kutimua vumbi siku za usoni huku waandaji wa Tamasha hilo wakionekana kujipanga zaidi ndani ya mwaka huu.
Meneja Mawasiliano wa wa Tigo Woinde shisael akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu Uzinduzi msimu mpya tamasha la Muziki la Tigo Fiesta 2019 kushoto kwake ni Mwenyekiti wa kamati ya Fiesta Sebastian Maganga katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika mapema jana katika ofisi za Clouds Media Group.
Mwenyekiti wa kamati ya Fiesta Sebastian Maganga akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa. Uzinduzi msimu mpya tamasha la Muziki la Tigo Fiesta 2019 mkutano huo ulifanyika katika ofisi za Clouds Media Group.
Uzinduzi msimu mpya tamasha la Muziki la Tigo Fiesta 2019 likiwa na maandalizi lukuki ikiwemo burudani na promosheni kabambe.
Shangwe zikiendelea mara baada ya Uzinduzi msimu mpya tamasha la Muziki la Tigo Fiesta 2019 likiwa na maandalizi lukuki ikiwemo burudani na promosheni kabambe