Burudani

Picha: CNN wafanya interview na Diamond, Dar

Sio kitu kilichozoeleka kwa shirika la habari maarufu duniani CNN kumfuata msanii wa Afrika nchini mwake kwaajili ya kumhoji.

11934827_1907541949471970_452148012_n
Diamond akiwa na mwandishi na cameraman wa CNN

CNN wametua Dar na kufanya interview na muimbaji wa Nana, Diamond Platnumz. Staa huyo ameshare picha kwenye mtandao wa Instagram na kuandika: Thanks alot @CNN it was a great interview….”

Haijulikani kama waandishi hao wa CNN walikuja Dar kwaajili ya interview pekee na Diamond lakini kuna uwezekano mkubwa kuwa wapo nchini kwaajili ya kuripoti masuala ya uchaguzi na wametumia fursa hiyo kumhoji.

Wakati huo Diamond ameshare picha hiyo chini na kunukuu maneno ya John Lennon: When I went to school they asked me what I wanted to be when I grew up, I wrote down HAPPY. They told me I didn’t understand the assignment and I told them they didn’t understand LIFE Happy Maulid … #TheChibus.

11887024_160669154275261_1328867283_n

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents