Picha: Dola milioni 1 zapukutika kwenye sherehe ya birthday ya Mugabe
Kiasi cha dola milioni moja za Marekani, zimetumika kuandaa sherehe ya siku ya kuzaliwa ya Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe aliyetimiza umri wa miaka 91.
Sherehe hiyo ilifanyika Jumamosi iliyopita kwenye hoteli ya kifahari (Elephant Hill) iliyopo karibu na maporomoko ya Victoria katika mto Zambezi.
Rais Mugabe ndiye kiongozi mwenye umri mkubwa kuliko wote duniani huku akitarajia kuwania nafasi nyingine hadi mwaka 2018. Wafuasi wake katika chama tawala cha ZANU-PF wameahidi kuendeleea kumuunga mkono kiongozi wao aliyetawala tokea walivyopata uhuru.
Wamesema wataendelea kumpa nafasi kwa kipindi kingine bila kujali afya yake ambayo imeendelea kuzorota kila siku bila kusahau kudondoka kwake siku chache zilizopita huku akiwarushia lawama walinzi wake kwa kutokuwa makini na kazi yao.
Kwenye sherehe hiyo, watu walikula na kunywa vya kutosha katika birthday hiyo kubwa na keki nyingi za kutosha zilikatwa huku mzee huyo akitumia siku huyo kuwarushia lawama na shutuma nyingi Wamarekani.
Vile vile Kiongozi huyo aliingia akiwa kwenye gari la kifahari la zamani lililotengenezwa mwaka 1955, Ford Modeo.
Chama cha upinzani nchini humo hakikukubaliana na sherehe hiyo iliyotumia fedha nyingi za umma huku watu wengi wakiwa kwenye umaskini na huduma mbaya kwenye hospitalini.