Titanic yatwaa nafasi ya kwanza katika Safari Lager Nyama Choma Competition 2013
Baa ya Titanic kutoka Vingunguti jijini Dar-Es-Salaam, Jana jioni iliweza kunyakua ushindi wa kwanza katika shindano la Safari lagaer Nyama Choma Competition 2013, katika fainali iliyofanyika katika viwanja vywa Leaders Club jijini Dar-Es-Salaam.
Shindano hilo ambalo jana lilifikia kilele chake lilizikutanisha baa tano ambapo kati ya hizo, baa ya Fyatanga ilichukua ushindi wa pili na ushindi wa tatu ulienda kwa baa ya Asenga na Soccer City ilichukua nafasi ya nne wakati baa ya Uhakika ikishika nafasi ya tano. Baa zote ikiwemo ya Titanic zilijishindia tuzo za kuanzia shilingi milioni moja kwa mshindi wa kwanza, laki nane kwa mshidi wa pili, laki sita kwa mshindi wa tatu, laki nne kwa mshindi wa nne na kiasi cha shilingi laki mbili kwa mshindi wa tano, ambazo zilikabidhiwa na mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Ilala Bwana Raymond Mushi akishuhudiwa naye meneja wa kinywaji cha Bia ya safari lager ambao ndio wadhamini wakuu wa shindano hilo la Safari Lager Nyama Choma competition 201, Bwana Oscar Shelukindo.
Angaia picha za hapa chini